Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Marais wawili walivyoondolewa madarakani

Jumanne , 2nd Mar , 2021

Ndani ya miaka 10, marais wawili wa klabu ya soka ya Barcelona ya Hispania, Sandro Rosell na Jose Maria Bartomeu hawajamaliza awamu zao za uongozi. Wameondolewa madarakani kwa shinikizo na kisha kushtakiwa.

Jose Maria Bartomeu (kushoto) na Sandro Rosell (kulia)

Mwaka 2010 mfanyabiashara Sandro Rosell, aliingia madarakani lakini mwaka 2014 akaondolewa kwa shinikizo na kulazimika kujiuzulu na baadaye alishtakiwa na kufungwa jela lakini baadaye aliachiwa huru.

Alituhumiwa kwa matumizi mabaya ya pesa na madaraka, lakini pia utakatishaji wa fedha zaidi ya €20 million, ikiwemo usajili wa Neymar Jr kutoka Santos.

Sandro Rosell

Mwaka huo 2014 aliyekuwa Makamu wake wa Rais Jose Maria Bartomeu, akashika hatamu hadi Oktoba 2020, ambapo alilazimika kujiuzulu kwa shinikizo huku akikumbana na tuhuma mbalimbali ikiwemo matumizi mabaya ya pesa pamoja na madaraka.

Jana Machi 1, 2021 amekamatwa na atafunguliwa mashtaka ambayo kwa kiasi kikubwa yanatajwa ni kuajiri watu wa mitandao kwaajili ya kuwachafua wachezaji wa zamani na wasasa pamoja na viongozi waliokuwa wanapinga utawala wake.

Jose Maria Bartomeu

Uchaguzi wa Barcelona utafanyika Machi 7, 2021 na wagombea watatu wenye nguvu ni Rais wa zamani wa klabu hiyo Joan Raporta, Wafanyabiashara Victor Font na Toni Freixa.
 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa