Jumanne , 13th Aug , 2024

Juma Ally Magoma na Geofrey Mwaipopo, wamekamatwa kwa kosa lilofunguliwa na mwanasheria wa Yanga Simon Patric, kudai wamegushi nyaraka.

Jacob Masenene, wakili wa upande wa Magoma na Mwaipopo ambaye amesema kosa walilokamatwa nalo linadhaminika na wao wamekamilisha taratibu zote za kupata dhamana.

Magoma na Mwaipopo wamekamatwa leo baada ya kutoka Mahakama Kuu, kusikiliza rufaa kesi yao dhidi ya bodi ya wadhamini wa Yanga, ambayo imeahirishwa mpaka tarehe 21 mwezi Agosti ambapo upande wa bodi ya wadhamini wa Yanga watakuwa wameshapata wito