Jumatatu , 27th Jun , 2016

Mchezaji nyota duniani Lionel Messi ametangaza rasmi kustaafu kuichezea timu ya taifa ikiwa ni baada ya kukosa penati, wakati Argentina ikishindwa kutwaa kombe la Copa America dhidi ya Chile.

Messi amechukua uamuzi huo wakati timu ya soka ya taifa ya Argentina ikiwa imepoteza ushindi mara nne katika miaka tisa kwenye michuano mikubwa ya kimataifa.

Mchezaji huyo amesema kwake yeye basi tena hatochezea timu ya taifa, na kuongeza kuwa amefanya kila awezalo na inauma sana kutokuwa bingwa wa Copa America.

Katika klabu yake ya Barcelona, Messi ameshinda ubingwa wa ligi ya Hispania La Liga mara nane na Ligi ya Mabingwa wa Ulaya mara nne. Kwa timu ya taifa Messi alishinda medali ya dhahabu katika Olimpiki mwaka 2008.