Jumanne , 16th Mei , 2017

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Young Africans leo wanashuka dimbani kuvaana na Toto Africans FC huku wakimkosa kiungo mshambuliaji Saimon Msuva baada ya kupata majeruhi mechi iliyopita dhidi ya Mbeya City.

Pamoja na hayo, uongozi wa Yanga umekitaja kikosi chake kizima kinachoenda kutafuta alama tatu za kukamilisha ushindi wao katika uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.

1. Beno Kakolanya 
2. Hassan Kessy
3. Haji Mwinyi 
4. Kelvin Yondani 
5. Vincent Bossou
6. Thaban Kamusoko
7. Juma Mahadhi. 
8. Haruna Niyonzima
9. Amisi Tambwe 
10. Obrey Chirwa 
11. Geofrey Mwashuiya 
Akiba
Deogratius Munishi, Juma Abdul,Nadir Haroub, Matheo Antony, Deusi Kaseke , Emmanuel Martin pamoja na Justine Zulu.