Jumapili , 30th Oct , 2016

Winga wa Simba, Shiza Kichuya ameendelea kuwatesa makipa wa timu zinazoshiriki Ligi Kuu Bara baada ya jana kuziona nyavu wakati Simba ikishinda 3-0 dhidi ya Mwadui FC, hivyo kuzidi kuwaacha wapinzani wao wakiwanyoshea kidole kileleni. 

Shizza Kichuya

Katika mechi hiyo iliyopigwa Uwanja wa CCM Kambarage , Shinyanga jana, Kichuya alifunga bao la pili dakika ya 44 na kumfanya afikishe bao lake la nane msimu huu. Simba ilishinda kwa mabao 3-0.