Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

John Bocco: Yanga hawatoki!

Jumatatu , 3rd Mei , 2021

Nahodha na mshambuliaji wa klabu ya Simba, John Rafael Bocco amejinasibu kuwa wataibuka na ushindi mbele ya watani wao wa jadi, klabu ya Yanga siku ya Jumamosi Mei 8, 2021 kwenye mchezo wa Ligi kuu bara utakaochezwa kwenye dimba la Mkapa jijini Dar es Salaam.

Mshambuliaji na Nahodha wa klabu ya Simba, John Rafael Bocco.

Bocco ameyasema hayo baaada ya Simba kutinga hatua ya robo fainali ya kombe la Shirikisho la Azam kwa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Kagera Sukari jijini Dar es Salaam huku akiwashukuru mashabiki wa Simba kwa kuwa na moyo wa kuwaunga mkono.

Bocco amesema, “Kuelekea mchezo huo, tunaamini mchezo utakuwa mgumu, lakini ni kujipanga tu tunaamini timu yetu ina wachezaji wazuri, wachezaji wazoefu kwa hiyo tunaamini tutapambana na tutaweza kupata matokeo mazuri katika huo mchezo”.

Bocco ambaye ameshaifunga Yanga mabao 10 alipokuwa anaichezea klabu ya Azam, ameizungumzia hali ya watani wake wa jadi, Yanga kwa kusema;

“Kwanza tunawaheshimu wapinzani, ni timu nzuri ukiangalia hata mwanzo wa msimu walianza vizuri na hata ukiangalia wanavyocheza wanacheza vizuri, lakini tunaamini upande wetu tutajipanga vizuri na tunaweza kupata matokeo mazuri ya alama tatu kwenye mchezo huo”.

Mchezo huo unaotazamiwa kuwa wenye upinzani mkali kutokana na wawili hao kuwa kwenye mbio za ubingwa wa VPL, Simba akiwa ni kinara akiwa na alama 61, alama nne mbele ya Yanga anayeshika nafasi ya pili akiwa mbele ya Simba kwa michezo miwili, akiwa ana michezo 27.

Mchezo huo ni wa mzunguko wa pili wa VPL baada ya sare ya bao 1-1 kwenye mzunguko wa kwanza, pia unataraji kuwa mchezo wa 108 baada ya wawili hao kukutana mara 107 kwenye michuano yote, Yanga akishinda michezo 37, Simba michezo 32 na kutoka sare michezo 38.
 

HABARI ZAIDI

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita