Jumatatu , 10th Mei , 2021

Rapper J. Cole anatarajiwa kushiriki  kwenye ligi kuu ya mpira wa kikapu ''Basketball Africa League'' nchini Rwanda inayotarajia kuanza siku ya Jumapili tarehe 16, Mei  na kumalizika Mei 3o,2021.

Msanii J. Cole

New Times Rwanda wamesema klabu ya Patriots imepanga kumtumia rapper huyo na tayari amejumuishwa kwenye kikosi kwa ajili ya michezo ijayo.

Cole aliwahi kucheza mpira wa kikapu kabla hajaingia rasmi kwenye muziki na alikuwa akifanya mazoezi kwa juhudi ili aje  kuwa mchezaji wa NBA Marekani hapo baadae lakini hakuwa hivyo.

BAL itachezewa Kigali Arena katika utaratibu wa makundi, timu 12 za mataifa 12 zinatarajiwa kushiriki mashindano hayo.