Jumapili , 9th Mei , 2021

Kitendo cha kuonekana kwa panya uwanjani humo imetajwa kua ni kashfa nyingine kwa wamiliki wa timu hiyo familia ya Glazer kwa kukataa kufanya ukarabati wa pauni milioni 200 na kuuacha uwanja huo wa kifahari wa Manchester United na kuwatia aibu kwa wapinzani wao.

Picha za sehemu ya jukwaa la Theater of Dreams na wachambuzi wa michezo akiwemo gwiji wa Man United Gary Neville wakizungumzia hali ya uwanja wa Klabu hiyo.

Uwanja huo uliopewa jina la ukumbi wa michezo wa Ndoto “Theatre of Dreams” na pia mchezaji wa zamani wa timu hiyo Gary Neville alioonyesha mara kadhaa kwa wiki kadhaa zilizopita, aliposema kwamba Old Trafford sio chochote kwasasa.

Katika kiwango cha juu, uwanja wa Old Trafford inaonekana kuwa uwanja mzuri wenye uwezo wake wa kuchukua watu elfu 76,000 na ndio uwanja wenye uwezo wa juu zaidi kwenye Ligi kuu ya England.

Hiyo sio kwa sababu ya Ole Gunnar Solskjaer kushindwa kutwaa taji la Ligi Kuu kwa mashabiki wa Manchester United, bali ni kosa la familia ya Glazer ambao ni kama wameutelekeza uwanja huo hadi kushika kutu na kuoza.