Jumanne , 26th Jan , 2016

Bingwa mtetezi wa michuano ya wazi ya Australia Novak Djokovic atakutana uso kwa uso na bingwa mara 17 wa grand slam kwenye mchezo wa nusu fainali wa michuano hiyo baada ya wote kushinda kwenye mechi za robo fainali.

Federer anayeshikilia nafasi ya tatu kwa viwango vya ubora duniani ametinga nusu fainali kwa kumshinda Tomas Berdyich kwa seti 7-6 (7-4) 6-2 6-4 .

Naye kinara kwa ubora duniani Djokovic ameendeleza harakati zake za kutaka kutetea taji lake baada ya leo kumshinda Kei Nishikori raia wa Japan kwa seti 6-3 6-2 6-4.

Mapema hii leo Serena William ambaye ni bingwa mtetezi wa michuano hiyo upande wa wanawake ameshinda mchezo wake dhidi ya Maria Sharapova na kutinga nusu fainali.