Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

BMT yataka nidhamu kwa mabondia

Jumanne , 17th Jan , 2023

Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) Neema Msitha, amewasihi mabondia nchini kuwa na nidhamu ili kuaminiwa na jamii pamoja na kuwavutia wadhamini kuwekeza katika mchezo huo

Msitha amesema hayo wakati akizungumza na bondia Pius Mpenda na ujumbe alioambatana nao walipotembelea ofisi za BMT kushukuru kwa ufadhiliwa tiketi 3 za ndege kurejea nyumbani baada ya kuibuka na ubingwa wa mkanda wa WBU - Afrika (Middleweight) katika pambano la round 12 lililofanyika nchini Uganda dhidi ya Bondia Farouk Daku.

Amesema kuwa, kufanya kwao vizuri kutasaidia kulipa fadhila kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Hassan Suluhu ambaye ameamua kuipa mchango wa kuiendeleza tasnia ya michezo hapa nchini.

“Tunawapongeza mabondia wachache ambao wamekuwa wanaiwakilisha nchi vizuri, lakini tumekuwa hatupati taarifa zao mbaya, hatukatai kunaweza kuwepo na changamoto kwa upande wa kamisheni ama Serikali ni vyema tukatumia njia nzuri ya kuwasilisha matatizo yetu,” amesema Neema.

Aidha amewaagiza Kamisheni ya Ngumi za kulipwa Tanzania (TPBRC) kuhakikisha mabondia wanakuwa na mameneja, na kuwataka wawe wanawaandalia semina wadau wao hao pamoja na makocha.

Kwa upande wake Bondia Pius Mpenda ameishukuru Serikali kwa kumpa sapoti ambayo hakuitarajia na ameahidi kuutumia mkanda huo kupambana na mabondia wa ndani na nje kuendelea kuonyesha ubora wake.

Naye Katibu Mkuu wa TPBRC Yahya Poli, alisema kuwa wana mpango wa kuendesha kozi ya waamuzi na makocha wa mchezo huo.

Meneja wa bondia huyo, Hassan Seta ameiomba Serikali kuendelea kusapoti wadau wa ngumi wenye vituo vya kukuza vipaji vya mabondia ili waweze kuibua vipaji zaidi.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa