Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mwasiti atoa wito kwa Nandy na Zuchu

Jumanne , 5th Jul , 2022

Staa wa bongo fleva, Mwasiti Almasi leo alifika katika ofisi za East Africa TV na East Africa Radio na kukabidhi mchango wa taulo za kike pakiti 72 kupitia kampeni ya Namthamini ambazo zitakwenda kusaidia wanafunzi 7 shuleni kwa mwaka mzima.

Mwasiti akiongea kwenye kipindi cha Mama Mia cha East Africa Radio siku ya leo.

Mwasiti ni miongoni mwa wasanii waliokuwepo katika uzinduzi wa kampeni ya Namthamini iliyofanyika Mei 27 mwaka huu katika shule ya sekondari Kidete, Wilaya ya Kigamboni, Dar es Salaam.

Hedhi imekua kikwazo kikubwa sana katika elimu ya mtoto wa kike, kwani wapo wanaoshindwa kwenda shule siku 3 hadi 7 kwa sababu ya maumivu makali wakati wa hedhi, na wengine kwa sababu ya ukosefu wa taulo za kike za kujihifadhi hivyo anaweza kubaki nyumbani hadi amalize hedhi.

Mwasiti anasema anatambua changamoto wanazokumbana nazo wanafunzi wa kike shuleni wakikosa taulo za kike za kujihifadhi katika kipindi cha hedhi, moja wapo ni kushindwa kufika shule.

Kampeni ya Namthamini imelenga kuwasaidia wanafunzi wanaotoka katika familia duni nchini kwa kuwapatia taulo za kike na kuhakikisha hawakosi tena masomo pindi wanapokuwa katika siku zao za hedhi na kuwaongezea uwezo wa kujiamini, kusoma kwa bidii na kutimiza ndoto zao.

Mwasiti ametoa wito kwa wasanii wa kike nchini kama Linah, Nandy, Dayna Nyange, Maua Sama, Haitham, Saraphina na Zuchu wajitokeze kuwasaidia wanafunzi wa kike waweze kupata mahitaji muhimu shuleni.

 

 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa