Tony anadai alifanyiwa tukio hilo mwaka 2019.
Baada ya kufukuzwa kazi alimfungulia kesi bosi wake wa zamani, kwa madai aliwahi kumfanyia unyanyasaji wa kijinsia mwaka 2019 akiwa kazini kwa kumdhihaki muonekano wake hana nywele kichwani.
Aliipeleka kampuni hiyo mahakamani akidai amekuwa mwathirika wa unyanyasaji wa kijinsia baada ya kugombana na msimamizi wa kiwanda hicho, Jamie King.
Tony ameshinda kesi yake baada ya jaji wa mahakama Jonathan Brain, kutoa uamuzi kuwa, kumwita mtu ana upara ni unyanyasaji katika eneo la kazi kwa mujibu wa sheria za ajira nchini Uingereza.