Alhamisi , 20th Apr , 2017

Msanii wa filamu nchini Yusuph Mlela amemtusi rapa Nay wa Mitego kwa kile anachodai kuwa msanii huyo anapotosha jamii juu ya maandamano waliofanya baadhi ya wasanii  wa filamu nchini.

Yusuph Mlela (Kushoto) na Nay wa Mitego

Yusuph Mlela ambaye kwenye post yake ameonekana kushindwa kutumia lugha ya staha huku akionesha kutokwa na povu jingi kutokana na mapokeo ya mashabiki wa filamu ambao walio wengi wamekuwa wakiwachana wasanii hao na kuwataka kufanya kazi zenye ubora.

Rapa Nay wa Mitego alisikika akisema kuwa baadhi ya wasanii wa filamu ambao waliandamana ni matahira kwani kitendo cha wao kutaka filamu za nje zizuiliwe hakina tija na mantiki yoyote.

Kutokana na jambo hilo, ndipo hapo msanii huyo alipoamua kushusha ujumbe kwa msanii Nay wa Mitego

Nay wa Mitego

"Nay True Boy wewe jamaa si ulikuwa chocolaa wewe leo umeyapatia kidogo unasahau kwamba nyuma yako kuna kundi la vijana wanatamani kuwa waigizaji\wanamuziki wakubwa....acha kupotosha jamii yetu Kwa sababu zako binafsi... sisi wasanii hatujakataza movie za nje. Tunataka wanaozisambaza wafuate taratibu za kisheria ili uwiano wa biashara uwepo ndiyo lengo la maandamano" alisema Mlela 

Mbali na hapo msanii huyo pia ameomba mpambano na Nay wazichape

"Nay wa Mitego acha kutafuta sifa... nakushangaa kuwa na ufikilivu mdogo kama wewe siyo msanii...halafu huwezi kufananisha filamu na muziki..... Wewe si mtoto wa Manzese unajifanya unajua kupiga ngumi nataka Round 3 tu za boxing kwenye stage ili Tanzania ijue nani taahira nikutie adabu..... This is serous coz we mtoto mdogo tu kwangu ********** kuongea sana tabia za kike wewe si hip hop na unajiamini njoo uwanjani chagua popote pale" Yusuph Mlela