Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wasanii hawa walitamani jukwaa la EATV AWARDS

Jumapili , 16th Oct , 2016

Tuzo kubwa za muziki na filamu zinazotarajiwa kufanyika kwa mara ya kwanza tar 10 Desemba 2016 jijini Dar es salaam Tanzania, zimeleta hamasa kubwa wasanii wa nchi za Afrika Mashariki wakisema ni neema kwao, huku wengine wakilitamani jukwaa lake.

Peter Msechu (Kushoto), Crazy GK (Kulia)

Wakizungumza na East Africa TV na East Africa Radio kwa nyakati tofauti tofauti, baadhi ya wasanii wamesema wapo tayari kutoa burudani siku ya kutolewa kwa tuzo hizo, burudani ambayo itaandikwa kwenye historia ya EATV AWARDS.

Kwenye kipindi cha Planet Bongo kinachorushwa na East Africa Radio, msanii Peter Msechu alisikika akisema iwapo hatakuwa nominated kwenye tuzo hizo, anatamani apewe fursa ya kutoa burudani ambayo itaacha historia kwake na kwa mashabiki.

"Yani acha niseme tu kwa kweli, hata nisipokuwa nominated au kushinda hizo tuzo, basi naomba nipewe fursa ya kuperfom kwenye EATV AWARDS, na siku hiyo nawaambia nitatoa burudani ya kufa mtu, kwa mara ya kwanza nitaperfom tumbo wazi, nitavua shati ili watu wote waone litumbo langu siku hiyo, naitamani hiyo siku kama nini", alisema Peter Msechu.

Naye msanii mkongwe wa rap hapa bongo ambaye alikaa kimya kwa muda mrefu na kurudi kwa kishindo, King Crazy GK, amesema anatamani angeperfom kwenye sherehe za utoaji wa tuzo hizo, kwani itakuwa ni furaha kubwa kwake.

"EATV AWARDS tunaisubiria kwa hamu, na natamani yani natamani sana, achana na kupata tuzo, japo hata kuperfom katika tukio kama hilo", alisema King Crazy GK.

EATV AWARDS ndio tuzo kuwa za kwanza kuanzishwa na media Afrika Mashariki, ambazo zitahusisha wasanii wa filamu na muziki wa nchi za Afrika Mashariki moja kwa moja.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa