
Hivi sasa Mr T-Touch anauguza majeraha baada ya kupata ajali mbaya ya Bajaji ambayo nusura ichukue maisha yake, akiumia katika maeneo ya bega na kichwani wakati akiwa anatoka Coco Beach.
Mr T-Touch ameiambia enewz kuwa alikuwa amepanda Bajaj pamoja na Msanii wake mmoja anayefahamika kwa jina Bija, na tukio hili baya lilisababishwa na mwendokasi wa dereva huyo wa bajaj.