Ijumaa , 31st Oct , 2014

Onesho kubwa kabisa la Mitindo Afrika Mashariki na kati, Swahili Fashion Week 2014 linatarajiwa kufanyika tarehe 5 mpaka 7 mwezi Desemba mwaka huu jijini Dar es Salaam, hii ikiwa ni mwaka wake wa 7 mfululizo.

Kwa mwaka huu, onesho hili linatarajia kuwaleta pamoja wabunifu mavazi 24 tofauti kuonesha kazi zao za ubunifu kwa siku 3 mfululizo.

Onesho hilo pia linatoa nafasi wa wabunifu wanaochipukia kupata jukwaa la kuonesha vipaji vyao ambapo kutakuwa na shindano la kuwapambanisha uwezo wao.