Jumanne , 26th Mar , 2024

Moja ya taarifa kubwa Marekani zinamuhusu mwanamuziki wa HipHop #Diddy kuvamiwa na Idara ya Usalama wa Taifa nyumbani kwake Los Angeles na Miami.

Picha ya Diddy

Watu hao wa Usalama wa Taifa Marekani waliwapiga pingu watu watatu waliowakuta nyumbani kwa Diddy wawili kati ya hao ni watoto wake Christian Combs na Justin Combs.

Chanzo cha Usalama kuvamia nyumbani kwake ni uchunguzi wa madai ya kesi zinazomkabili za unyanyasaji wa kijinsia na biashara ya ngono.

Baada ya taarifa hizo Diddy alionekana uwanja wa Ndege wa Miami, na ndege yake binafsi kufuatiliwa mpaka visiwa vya Caribbean.