Msanii Mr Seed
Wakati yupo mapumziko na mke wake “Nimoh Gachuiri” huko pwani ya Kenya alitumia muda huo kukanusha taarifa zilizokuwa zikiendelea kusambaa juu ya mwanamke aliyekuwa akimtuhumu kuwa alikataa mimba yake na kumlazimisha aitoe.
Seed amesema kuwa siku zote ni mwenye furaha bila kujali mambo yanayotokea maishani mwake, licha ya kashfa za ngono kuendelea kumuandama za kutoka kimapenzi na warembo tofauti tofauti.