Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mke wa Roma adai hawezi kurudia tena

Ijumaa , 11th Aug , 2017

Baada ya kufanya kazi kubwa ya kumuwakilisha mume wake katika kutambulisha wimbo wake mpya 'Zimbabwe' Mke wa Roma Mkatoliki , Nancy amefunguka na kuweka wazi kwamba hii ndiyo itakuwa kazi yake wa kwanza na mwisho kwani hana kipaji cha kazi ya sanaa

Roma akiwa na mkewe Nancy anayemlisha Keki

Nancy amefunguka hayo wakati akifanya mahojiano na mwandishi wetu na kusema hana kipaji na uelewa mkubwa wa kazi za muziki lakini pia asingeweza kuacha kumsaidia mume wake katika kumuwakilisha kwenye vyombo vya habari ingawa ni kazi ambayo hadhani kama ataweza kuendelea nayo wakati mwingine.

"Siwezi kuendelea na hii kazi kwani mimi sina kipaji cha kazi hii kama usambazaji wa kazi hizi na idea ya muziki lakini kazi hii imekuja bahati mbaya na nimesimama kama muwakilishi na nimesimama kwenye hiyo nafasi" alisema Nancy

Aidha baada ya kuibuka maswali mengi kuhusu aina ya utambulishaji wa ngoma mpya ya msanii Roma Mkatoliki, Nancy amefunguka kwamba mumewe alishindwa kuacha kuachia wimbo huo kutokana na ukweli kwamba mume wake alishaweka maombi ya Interview kwenye vingi vya habari hivyo isingekuwa busara kutotokea. 

"Alishaomba interview kwenye vyombo vya habari kwamba hii wiki atakuwa na kazi mpya lakini akapata safari ya ghafla kwenda huko Zimbabwe na kwa sababu kuanza ku - cancell hizi interview ni kazi kubwa sana hivyo imenibidi mimi nibebe jukumu hili na kulisimamia ili yeye atakaporudi aendelee mimi nitakapoishia".

Aidha Mke wa Roma ameongeza kuwa "Mapokezi niliyoyapata ni tofauti na matarajio yangu kwani mimi sipo sana katika mambo ya muziki kwa sana lakini mapokezi ni makubwa sana na wimbo umeshaanza kufanya vizuri.

Bonyeza hapa kumsikiliza zaidi Nancy, Mke wa Roma

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa