Jumanne , 6th Oct , 2015

Nyota wa muziki wa injili hapa nchini, Emmanuel Mbasha ameiambia eNewz kuwa kutokana na nafasi yake katika sanaa,
anashiriki katika harakati za kuiombea nchi ya Tanzania amani katika kuelekea uchaguzi Mkuu mwishoni mwa mwezi huu.

Nyota wa muziki wa injili hapa nchini, Emmanuel Mbasha

Mbasha amewataka pia watanzania na mashabiki wake kufahamu kuwa kwa sasa mbali na kujikita kuombea amani, kutokana na kuwa na muda na akili iliyotulia baada ya kufanikiwa kumaliza kesi yake, amewekeza nguvu katika kufanya video na pia kuisukuma albam yake mpya Haribu Mipango ya Shetani.

Mbasha ambaye hakutaka kuongelea masuala binafsi ya familia yake kwa sasa, akionekana mwenye furaha amesema kuwa amani ya nchi, vilevile kazi zake za muziki ndio kitu alichoweka mbele kwa sasa kama anavyoeleza hapa.