Alhamisi , 3rd Dec , 2015

Nyota mkongwe katika gemu ya Bongofleva, Matonya amesema kuwa ili kukuza muziki hapa Bongo, kunahitajika wasanii kuongezeka zaidi wakiwa pia na juhudi binafsi zinazoeleweka katika kiwango kinachotakiwa.

Nyota mkongwe katika gemu ya Bongofleva, Matonya

Matonya pia ametoa ushauri huo kwa chipukizi, akiwataka kabla ya kuanza kutafuta msaada, wao binafsi wanapaswa kuanzisha mikakati, muonekano na malengo ya kuingia katika sanaa hiyo.