Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

MAKUNDI 5 YAPENYA FAINALI DANCE 100%

Jumatatu , 21st Sep , 2015

Baada ya mpambano wa kukata na shoka, hatimaye makundi matano ya kudansi Team ya shamba, Best Bo

Baada ya mpambano wa kukata na shoka, hatimaye makundi matano ya kudansi Team ya shamba, Best Boys, Team Makorokocho, The WD na The winners wamefanikiwa kuingia fainali ya mashindano makubwa ya Dance 100% (2015), baada ya kufanikiwa kujivunia alama zaidi katika mashindano hayo yaliyofanyika Don Bosco Oysterbay jijini Dar es Salaam siku ya juzi (Jumamosi).

Ushindani mkali ulionyeshwa na washiriki wote juu ya jukwaa la kisasa, ubunifu katika mitindo ya kucheza na mavazi kwa makundi hayo ukiwa ni kiburudisho kingine kikubwa kwa umati mkubwa uliohudhuria mashindano hayo.

Hisia nzito na huzuni vilitawala wakati wa kutangazwa kwa washindi, na kufikia wengine kupoteza fahamu hususana kwa makundi, ambayo hayakuweza kupenya wakiwepo Cute Babies, Quality Boys, The Best, Wazawa Crew na Majokeri.

Katika kuzingatia vigezo, haki, umakini na kusimamia sheria katika ubora wake hadi kuhakikisha washindi waliopatikana wanastahili, dawati la waamuzi ambalo limezoeleka kuendeshwa na majaji Super Nyamwela, Queen Darleen pamoja na Shetta liliongezeka majaji wawili wapya, Mwalimu mahiri wa Dansi Kalila Mbowe na Lydia Igarabuza kutoka EATV.

Baada ya mzunguko huo, sasa macho ni kwenye hatua ya fainali ambapo mabingwa wapya wa kombe la Dance 100% watapatikana na kuheshimika kama wafalme wa dansi Tanznia. Vilevile mabingwa hao watashinda zawadi tofauti ikiwemo kitita cha fedha taslim shilingi milioni 5 za Tanzania. Swali kubwa likibaki kuwa ni kundi gani litakaloibuka na taji hili na kitita hicho mwaka huu.

Usikose kutazama kila kilichojiri katika hatua ya Nusu Fainali ya mashindano hayo yaliyoshereheshwa kwa uzuri kabisa na T Bway 360 na Maggie Vampire kwa kutazama kipindi cha Dance 100% kupitia EATV pekee, Jumamosi saa 12:30 jioni.

Safari inazidi kukaribia ukingoni kuelekea hatua ya fainali ambapo mashindano haya makubwa yanaletwa kwako na East Africa Television na East Africa Radio kwa udhamini mkubwa wa Vodacom Tanzania, na pia Cocacola kinywaji rasmi cha Dance 100% kwa mwaka huu kinachokupa sababu Bilioni za kujiamini.

Ni Burudani mwanzo mwisho, Dance 100% (2015).

HABARI ZAIDI

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa