Jumatatu , 19th Jul , 2021

Mchekeshaji Pili Kitimtim amelikataa jina la 'Slay Queen' kwa sababu wadada wanaojiita jina hilo huwa hawana akili na maisha yao yanaenda kibahati nasibu.

Picha ya Pili Kitimtim

Kupitia EATV & EA Radio Digital Pili Kitimtim anasema "Mimi sio Slay Queen cha kwanza, Slay Queen ni dada ambaye hana akili anatagemea maisha yake yaende kibahati nasibu, mimi napambana"

"Tuache zama za kishamba, mwanamke anaweza akafanya kazi, akanunua gari, na nyumba bila ya kumtegemea mwanaume, asilimia 98 wanawake wamejiajiri na wajasiriamali hivyo wakiona mwanamke kafanikiwa wasione kama mambo ya kudanga au sponser"

Zaidi mtazame Pili Kitimtim akizungumzia zaidi suala hilo.