Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Luffa atoa onyo kali

Jumatatu , 24th Jul , 2017

Mtayarishaji wa muziki King Lufa amewataka wasanii kutoka 'Switcher Music Group' kuheshimu kipaji chake na kuwafahamisha kuwa muziki ni biashara kama zilivyo nyinginezo.

Lufa amelazimika kutoa kauli hiyo kwa madai ya kuwa kundi hilo limetoa nyimbo tatu alizozitengeneza wakati akifanya kazi kwenye studio ya switch na kusema kwamba anashangaa kazi zake kutoka bila makubaliano yoyote.

"Mimi muziki ni kazi yangu, na huwa sikubaliani na watu wanaotaka kunirudisha nyuma. Ni kweli mimi sasa hivi nipo Wanene lakini kuna kazi zangu nyingi niliziacha kwa Switcher nilioondoka cha kushangaza wanaendelea kutoa kazi nilizozitengeneza mimi. Wao wanazidi kunufaika kimuziki Halafu mwenye midundo sina taarifa siyo busara," alifunguka

Ameongeza kuwa "Sasa hivi nafanya biashara hakuna tena ile kupeana kazi kiushkaji. Hata kama kuna ugomvi hayo ni mambo yanayokujaga na kupita, kila moja aheshimu kazi ya mwenzake kwa sababu mwisho wa siku mimi na wao tunategemeana kwani hakuna msanii bila prodyuza. Tusichukuliane poa," aliongeza Lufa.

Kuachana na hayo mtayarishaji huyo nyimbo kubwa mbalimbali hapa nchini amewataka wasanii kuhakikisha wanajiongeza kutoka sehemu moja kwenda nyingine haswa wanapokuwa wakifanya shoo na kutotegemea kuimba kwa kutumia CD.

"Wasanii wetu wajiongeze, wao ndiyo watu wanaoutangaza muziki wa Tanzania hivyo ni vizuri wakabadilisha mifumo ya kufanya show, waanze kuimba hata 'Live' ili kupambana na wenzetu waliopiga hatua kimuziki. Wapige mazoezi ya kutosha," amesema
 

HABARI ZAIDI

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe