
Msanii huyu ameibuka na kukanusha taarifa za yeye kufukuzwa katika nyumba yake aliyopanga huko Lagos, na kusema kuwa hii ni uzushi ambao mwenye nyumba wake ameamua kuupakaza kumchafulia jina kupitia vyombo vya habari.
Mvutano huo tayari umeripotiwa kufika mahakamani na sasa kila mmoja amekuwa na hamu ya kufahamu ni nini itakuwa hatma ya kesi hii yenye utata mkubwa.