Jumatatu , 1st Jul , 2019

Mastaa wawili kutokea nchini Nigeria na Africa kwa ujumla Davido na Wizkid, wamemaliza utata wao baada ya kupanda kwenye jukwaa moja.

Davido na Wizkid

Wawili hao walikua pamoja jijini Amsterdam nchini Uholanzi wikiendi iliyopita kwa shughuli zao tofauti. Davido alienda kwa ajili ya tamasha na Wizkid alikua anazindua bidhaa zake za nguo.

Davido alienda katika uzinduzi wa nguo wa  Wizkid , na Wizkid alienda kwenye tamasha la Davido na kuimba pamoja nyimbo zao.

Mastaa hao wameondoa utata uliokuwepo kwa mashabiki zao, kwamba wanatofauti kutokana na ushindani mkubwa  walionao katika muziki.