
Mwimbaji Cindy na Joel Atiku
Shughuli hiyo ya jadi iliyohudhuriwa na watu wachache ikijumuisha marafiki wa karibu na wana familia, imehalalisha ndoa yao baada ya mwaka mmoja wa uchumba wa wawili hao, huku harusi kamili ikitarajiwa kufungwa muda wowote kuanzia sasa.
Cindy amesema mipango sasa inaendelea ili harusi yao ifanyike na amesisitiza kuwa itafanyika mwaka huu.