Jumatatu , 2nd Oct , 2023

Kupitia page ya Instagram ya Queen Beyoncé ameachia Trela ​​ya filamu itakayoonesha matukio yote yaliyo tokea kwenye Tour yake ya "Renaissance World" na filamu hiyo itakuwa kwenye kumbi za sinema kuanzia mwezi Disemba.

Picha ya Queen Beyonce

Renaissance World ni ziara ya tisa kwake iliyoanza kufanyika  May 10, 2023 huko Stockholm, Sweden  na kumalizika jana Oktoba 1 huko mjini Kansas City.

Tour hiyo ilihusisha jumla ya show 56 kwenye miji tofauti tofauti duniani na imefanikisha kuingiza  kiasi cha ($461.2 million) zaidi ya TSh. Trilioni 1.1 ambapo watu milioni 2.2 walihudhuria maonesho yake.

Ikumbukwe kuwa hii ndio ziara kubwa na iliyotengeneza pesa ndefu kwa msanii wa Kike kwenye historia.