
Waziri wa Maliasili na Utalii Mohamed Mchengerwa
Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Maliasili na Utalii Mohamed Mchengerwa bungeni wakati akiipongeza timu hiyo kwa kuendelea kuitangaza vyema nchi baada ya kushika nafasi ya pili kwenye fainali za Kombe la Shirikisho Barani Afrika sambamba na kutoa mfungaji bora na golikipa bora wa mashindano hayo.
"Sambamba na hilo niwakaribishe pia mashabiki wote wa Yanga kwenda kujumuika pamoja na wachezaji hao katika safari hiyo katika tarehe itakayotangazwa na utaratibu utakaowekwa, ziara hizo tunapendekeza iitwe, “The CAF Finalists Royal Tour," amesema Waziri Mchengerwa
Aidha Waziri Mchengerwa amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye kwa kujitoa kwake kupitia filamu ya The Royal Tour ilivyoleta mafanikio lukuki nchini si tu watalii kwa kuongezeka, lakini pia nchi sasa ni kivutio cha mastaa mbalimbali na watu mashuhuri ambao wamekuwa wakija.