Jumamosi , 25th Nov , 2017

Aliyekuwa waziri wa fedha wa Zimbabwe chini ya utawala wa Mugabe, Ignatius Chombo, amefikishwa mahakamani leo akikabiliwa na mashataka ya rushwa.

Chombo alikuwa miongoni mwa watu waliokamatwa na jeshi wakati lilipochukua madaraka kabla ya kujiuzulu Mugabe wiki hii.

Wakili wa Chombo, Lovemore Madhuku amesema mteja wake alikuwa amelazwa hospitali hapo jana akiwa na majeraha yaliyotokana na kipigo alichopigwa na jeshi akiwa kizuizini.