Waziri wa Maji Jumaa Aweso
Akizungumza baada ya kutembelea chanzo cha maji cha Omururongo kilichoko wilayani humo, Waziri Aweso, amesema kuwa timu ya wataalamu kutoka wizarani inapaswa kuwasili Jumatatu ya leo katika wilaya ya Karagwe, na kuanza kushughulikia tatizo hilo.
Wakizungumza katika mkutano wa hadhara mbele ya Waziri huyo, baadhi ya wakazi wa miji ya Kayanga na Omurushaka, iliyoko wilayani humo wamesema kuwa wanakabiliwa na tatizo la uhaba wa maji, hali inayosababisha kununua ndoo moja ya maji yenye ujazo wa lita 20 kwa kati ya shilingi 500 hadi 1,000 kutoka katika visima vya watu binafsi.