![](http://eatv.tv/sites/default/files/styles/detailpageimg/public/news/2024/03/27/Untitled-1.jpg?itok=zZ5lNVJA×tamp=1711571712)
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Iringa ACP Allan Bukumbi
Akithibitisha kuwakamata watuhumia hao Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Iringa ACP ALLAN BUKUMBI amesema katika uchunguzi wa awali umebaini watuhumiwa hao ambao ni wakazi wa kimara Jijini Dar es Salaam wametengeneza bidhaa hizo kupitia kiwanda bandia cha kilimanjaro Wine ambacho uchunguzi unaendelea kubaini mahali kilipo.
Katika hatua nyingine pia kamanda Bukumbi amesema jeshi hilo pia linawashikia watu saba kwatuhuma za kukutwa na mali mbalimbali za wizi ikiwemo pikipiki nne ,runinga aina tofauti sabufa na vitu vingine ambapo watuhumiwa wote wamefikishwa mahakamani.