Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dkt. Pindi Chana.
Hayo yamesema na Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dkt. Pindi Chana, wakati akizungumza kwa njia ya mtandao kwenye mkutano wa kujenga uelewa kuhusu zoezi la uwekaji wa alama za mipaka katika Pori Tengefu la Loliondo na zoezi la uhamaji wa hiari la wakazi wa Ngorongoro
"Serikali yetu sikivu chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, inaendelea kujali maslahi ya wananchi kwa kutoa uhuru kwa wananchi walioamua kuhamia maeneo mengine kwa hiari yao,"amesema Waziri Chana
Waziri Balozi Dkt. Chana amesema ni ruhusa kwa wakazi hao kuchagua kwenda kuishi mahala wanapoona panafaa kwa kufuata taratibu zilizopo bila kuvunja sheria za nchi.