Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wachimbaji wadogo walia na Rais Magufuli

Jumanne , 28th Mar , 2017

Baadhi ya wachimbaji wadogo ambao wanadai kuwa ni sehemu ya wamiliki wa makontena yaliyozuiliwa katika bandari ya Dar es Salaam yakiwa na shehena ya mchanga wa madini, wameiomba serikali kupitia upya zuio hilo kwa maelezo kuwa limeathiri biashara.

Wachimbaji wadogo wadogo wanaosafirisha nje ya nchi mchanga wenye masalia ya madini wakizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam hii leo

Wakizungumza katika mkutano na wanahabari leo Jijini Dar es Salaam, wachimbaji hao wamesema kimsingi hawapingani na uamuzi huo wa serikali bali wanaunga mkono kwani uamuzi huo unaotokana na agizo la Rais John Pombe Magufuli alilolitoa takribani mwezi mmoja uliopita, linayalenga makampuni makubwa na siyo wao ambao ni wamachinga kwenye sekta ya madini.

Wamesema tangu lilipotolewa agizo la kutosafirisha nje mchanga wenye masalia ya madini, wamekuwa wakipata hasara kubwa ambapo mmoja wa wachimbaji hao amesema anaingia hasara ya zaidi ya shilingi milioni nne kwa siku kutokana na kusitisha shughuli za uchimbaji huku akitakiwa kulipia wastani wa dola ishirini kama gharama ya utunzaji kwa kila kontena linaloshikiliwa pale bandarini.

Sehemu ya makontena ya mchanga yanayoshikiliwa bandarini

Kwa mujibu wa maelezo ya wachimbaji hao akiwemo Bw. Mohammed Mkwayu anayemiliki kampuni ya Kambi Mineral Resources inayofanya shughuli zake wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma na Bw. King Selemani anayemiliki kampuni ya Wit Mining inayofanya shughuli zake wilaya za Kongwa na Mpwapwa; zaidi ya kontena sitini za wachimbaji wadogo wadogo zimezuiliwa zisisafirishwe kwenda nje ya nchi na kwamba hatua hiyo imechukuliwa huku wakiwa na vibali vyote vinavyowaruhusu kufanya biashara hiyo.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya