Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ukatili wa majumbani upingwe kwa nguvu-Henga

Jumanne , 6th Dec , 2022

Kituo cha Sheria na Haki za binadamu, wameiomba serikali kutunga sheria mahususi ya kupinga ukatili wa kijinsia au ukatili wa majumbani kwaajili ya kuhakikisha usalama zaidi wa wanawake dhidi ya ukatili wa kijinsia na ukatili wa majumbani.

Hayo ameyasema Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Anna Henga wakati akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam katika kuadhimisha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ambazo huadhimishwa kuanzia Novemba 25 hadi Disemba 10 .

Henga amesema kwa mwaka 2021 Tanzania imeshuhudia ongezeko la vitendo vya ukatili kwa wanawake na watoto wakiwa wahanga hivyo ameiomba serikali kuboresha huduma za jamii, haki na kuhakikisha wanawake wanapata msaada pale wanapofanyiwa ukatili.

"serikali iendelee kutoa elimu kwa jamii kuhusu hali za wanawake, watoto, wasichana na haki za binadamu kwa ujumla ili kuleta mabadiliko ya tabia lakini pia wanawake hao waweze kuwa na nyumba salama na huduma za kisaikolojia"

Aidha Henga amesema ukatili wa kimwili na ukatili wa kingono umeongoza zaidi ya ukatili mwingine hivyo ameiomba serikali kutunga sheria au sera kuruhusu watoto wanaopata ujauzito kurudi shule ili kukata gurudumu la umasikini litakaloendelea kuwaweka katika hatari ya kufanyiwa ukatili.

"Hili ni pamoja na kufuta au kurekebisha sheria zote zinazomnyima mtoto wa kike haki za kufurahia haki yake ya elimu ikiwemo sheria ya ndoa"

Vilevile Henga ameiomba serikali kuboresha elimu ili kuilinda jamii na mauaji yanayohusiana na mila na desturi.

"Mauaji ya wenza ni mauaji yanayotendwa na wenza wa mhanga awe mume, mchumba, mpenzi au mtu ambaye tayari kaachana na mhanga, ambapo utafiti uliofanywa na shirika la Afya Duniani ulionyesha kuwa asilimia 35 ya mauaji ya wanawake duniani yamefanywa na wenza na ilibainika kuwa ni asilimia 5 tu ya mauaji ya wanaume yanasababishwa na wenza wao"

Henga amezitaja changamoto ambazo zinaendelea kuongeza mauaji ya makusudi ya wanawake pamoja na ukatili wa kijinsia

"kuongezeka kwa ukatili dhidi ya wanawake na watoto, sheria kandamizi, kutokutekelezeka kwa sheria zilizopo, kutokuwepo kwa uhuru wa kiuchumi kwa Mwanamke, elimu ya teknolojia, ndoa na nafasi ya Mwanamke katika jamii, mila na desturi zilizopitwa na wakati, lakini pia wanawake wa vijijini"

Henga ameliomba jeshi la polisi kuendelea kuboresha mifumo ya ukusanyaji taarifa kuhusu mauaji ya makusudi ya wanawake na kutengeneza miongozo inayozingatia hali halisi hasa katika ukusanyaji wa matukio ya mauaji ya wanawake kwa kuyatenganisha na mauaji ya kawaida.

Mbali na hayo, Henga amesema endapo mifumo kandamizi na mila potofu ikiwemo fikra potofu zinazowanyima wanawake uhuru wa kutoa taarifa za ukatili ilibadilishwa, itasaidia kuwajengea uwezo watoa huduma ili watoe huduma rafiki kwa wahanga.

 

HABARI ZAIDI

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita