Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ujenzi 'Flyover' za Ubungo wazinduliwa

Jumatatu , 20th Mar , 2017

Ujenzi wa barabara za juu (Flyover) katika makutano ya barabara ya Ubungo umezinduliwa leo mara baada ya Rais wa Tanzania Dkt John Magufuli na Rais wa Benki ya Dunia Dkt. Jim Yong Kim kuweka jiwe la msingi.

Magufuli na Rais wa Benki ya Dunia Dkt. Jim Yong Kim wakifungua kitambaa ikiwa ni ishara ya kuweka jiwe la Msing la ujenzi wa barabara za juu (Interchange) kwenye makutano ya Ubungo March 20,2017

Barabara hizo za juu za ngazi tatu (Interchange), itagharimu kiasi cha Shilingi Bilioni 188.71 na itajengwa kwa muda wa miaka 3 na kuhusisha barabara za Nelson Mandela na Sam Nujoma ambapo takribani magari elfu 60 ambayo yatatumia barabara hizo kwa siku na kuwa mwarobaini wa msongamano wa magari katika makutano ya eneo la Ubungo.

Akihutubia katika uzinduzi huo, Rais Dkt. Magufuli amesema serikali yake inalenga kuboresha miundombinu ya barabara ili kurahisisha usafirishaji na kuchochea mapinduzi ya viwanda na kuweka wazi miradi mingi ya ujenzi wa barabara ambayo analenga kuijenga hivi karibuni na kuiweka Tanzania kwenye nchi ya uchumi wa kati.

Magufuli katika mazunzumzo Ikulu jijini Dar es salaam na Rais wa Benki ya Dunia Dkt. Jim Yong Kim kabla ya kwenda kuweka jiwe la Msing la ujenzi wa barabara za juu (Interchange) kwenye makutano ya Ubungo March 20,2017 

Kwa upande wake Rais wa Benki ya Dunia Dkt .Jim Yong Kim amesema, hatua hii ni ya kupeleka faida kwa jamii na kuchochea maendeleo yao, na kwamba Benki hiyo haiungi mkono miradi ya kizembe akitolea mfano ubinafsishaji ambao uliwahi kuleta hasara kwa jamii lakini sasa wanawezesha serikali kwa kutelekeza vipaumbele vya maendeleo na kuahidi kushirikiana na serikali ya Tanzania.

Naye Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa amewataka wakandarasi waliopewa tenda ya kujenga barabara hizo kutoa kipaumbele kwa watanzania kupata ajira katika ujenzi wa mradi huo, wenye lengo la kurahisisha usafiri katika Jiji la Dar es Salaam.

Magufuli na Rais wa Benki ya Dunia Dkt. Jim Yong Kim wakiwa wamepanda basi la mwendokasi huku wakibadilishana mawazo wakielekea Ubungo kuweka jiwe la Msing la ujenzi wa barabara za juu (Interchange) kwenye makutano ya Ubungo March 20,2017

HABARI ZAIDI

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita