
Basi lililomgonga Trafiki
Akieleza kuhusu tukio hilo Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Wilbroad Mutafungwa, amesema Askari huyo alisimamisha gari hilo kwa ajili ya ukaguzi, baada ya gari kukutwa na kosa na alimtaka dereva arudishe nyuma gari kwa ajili ya usalama, ndipo alimgonga askari huyo kwa nyuma na kusababisha kifo chake.
Hata hivyo Jeshi la polisi mkoa wa Mwanza limesema linamshikilia dereva wa gari hiyo ya shule ya msingi Nyamuge, Philipo Mhina kwa kutenda kosa hilo.