Tembo wakiwa katika hifadhi
Nchi za Afrika Kusini, Zimbabwe na Namibia zinaomba ridhaa ya chombo cha Kimataifa kuziruhusu kuuza hazina kubwa ya meno ya tembo waliyoyakamata, wakati Namibia ikitaka hatua ya kuzuia uuzaji wa meno hayo ya tembo iendelee.
Pia kumekuwa na mgawanyiko juu ya suala la uuzaji wa pembe za faru, ambapo Waziri wa Mazingira wa Zimbabwe, Oppah Muchuinguri akisema nchi yake inaungwa mkono na mataifa mengine ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC).