Jumatatu , 1st Jul , 2024

Mkuu wa mkoa wa Simiyu Kenan Kihongosi amepiga marufuku wanafunzi kutumikishwa kwenye mashamba binafsi ya walimu huku akiuagiza uongozi wa Halmashauri hiyo kufutilia suala hilo kwa ukaribu na hatua zichukuliwe kwa wale waliohusika.

Mkuu wa mkoa wa Simiyu Kenan Kihongosi, akizungumza na wananchi

Hatua hiyo imekuja mara baada ya kupokea kero hiyo kutoka kwa wananchi wa Kijiji cha Mwaukoli kilichopo Kata ya Kisesa wilaya ya Meatu mkoani hapo huku shutuma zikielekezwa kwenye shule ya msingi Mwaukoli.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri hiyo Khamis Masasi, ameahidi kuchukua hatua za haraka kwa wahusika ili iwe fundisho kwa wengine.