Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Rais Magufuli awachana wacheza utupu

Jumanne , 12th Dec , 2017

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amewataka watanzania kukemea vitendo vinavyodhihirisha mmomonyoko wa maadili, ikiwemo mabinti wanaocheza utupu kwenye video za muziki.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo wakati akizungumza kwenye mkutano wa Jumuiya ya Wazazi mjini Dodoma, na kusema kwamba huwa anashangazwa kila anapowasha Television kutazama muziki, na kukutana na mabinti wakicheza utupu huku wanaume wakiwa na mavazi ya staha, na kusema kwamba ni aibu kubwa kwa wazazi kuangalia mambo hayo.

“Mimi ni shabiki mzuri wa muziki, kila ukifungulia mziki wanaocheza utupu ni wanawake wanaume hapana., nyinyi kama jumuiya ya wazazi umefika wakati wa kukemea mambo haya, tunawafundisha nini watoto wetu, tunapenda mziki, lakini je, hiyo ndio muziki tunayocheza, tumeingiliwa na mdudu gani, saa nyingine unapoangalia TV na watoto wetu ni aibu kubwa, yanayofanyika pale ni aibu, si kwa sababu sitaki watu wastarehe, kama ni kwenye klabu kavue huko, lakini kwa nini uwavulie hata wasiohitaji kuona uc**? Tena kwa muda usio muafaka?”, amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli ameendelea kwa kuitaka jumuiya hiyo na watu wote kusimamia maadili, huku akivinyooshea mkono vyombo husika vinavyopaswa kushughulika na masuala ya utamaduni wa Mtanzania.

“Ifike mahali sisi kama watanzania, bila kujali vyama vyetu, tulinde maadili yetu, ninyi kama wazazi, sifahamu kama enzi za akina Fatma Karume au kina Maria Nyerere huo ndio ulikuwa mtindo, lakini nina uhakika enzi zile haikuwa hivyo, lakini vyombo vyetu vya habari, wasimamizi wa maadili haya wako wapi, wizara inayosimamia haya wako wapi, je, TCRA wako wapi, Niwaombe ndugu zangu Jumuiya ya wazazi kuikosoa hata serikali kwenye kusimamia maadili ya Tanzania”, amesema Rais Magufuli.

HABARI ZAIDI

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita