Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mwela aeleza mafanikio siku ya kwanza ya mkutano

Jumatano , 20th Oct , 2021

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya TEHAMA Tanzania Samson Mwela amesema siku ya kwanza ya Kongamano la Tano la Mkutano Mkuu wa Tehama 2021 imekuwa yenye mafanikio makubwa baada ya wawekezaji mbalimbali kukubali kushirikiana na serikali katika kukuza Tehama nchini.

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya TEHAMA Tanzania Samson Mwela (kushoto) akifanya mahojiano na Irene Tillya,

Mwela ameyasema hayo jioni ya leo Oktoba 20, 2021, kwenye mahojiano na EATVSaa1 yaliyoruka mojamoja kutokea Ukumbi wa Simba ndani ya Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), ambapo amesema huu ni mwanzo tu mengi zaidi yakuja.

‘’Kikubwa ambacho leo tumefanya ni mkutano na wawekezaji ‘Investors Round Table’ na hili jambo limeonekana #LIVE duniani kote, kiukweli kumekuwa na mafanikio makubwa sana kwasababu wameonesha nia ya kushirikiana na serikali kwenye kukuza Tehama nchini,’’ amesema Samson Mwela, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Tehama.

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya TEHAMA Tanzania Samson Mwela (kushoto) akiwa kwenye mkutano.

Aidha Mwela ameongeza kuwa, ‘’Siku ya leo imekuwa na mafanikio sana mwitikio wa watu umekuwa mkubwa sana, tunatarajia kesho watu watazidi kujitokeza zaidi kwasababu tunajadili masuala ya msingi hususani taifa na uchumi wa kidijitali jinsi gani watu watatumia Teknolojia kujiletea maendeleo,’’.

Kuhusu ujenzi wa taifa la kidijitali Mwela ameweka wazi kuwa, ‘’Tunafahamu suala la kodi linaonekana ni changamoto na limeongelewa, sasa jinsi gani taifa linufaike kupitia Tehama kwenye kukusanya kodi na tumekubaliana, jambo la msingi sasa ni kuangalia tu ni namna gani mifumo yetu itatumika,’’.

Washiriki mbalimbali wa mkutano wakiwa kwenye Ukumbi wa Simba ndani ya AICC.

Pia Mwela amedokeza kuhusu mjadala utakaoendelea kesho kwenye mkutano kwa kusema, ‘’Kesho tutaangalia uchumi wa kidijitali, jamii ya kidijitali na utawala wa kidijitali kwahiyo haya yote ni masuala ya msingi leo tumeanza tu ila kesho tutaendelea kwa upana wake,’’.
 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa