Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Msijenge nyumba kiholela- Dkt. Mabula

Alhamisi , 8th Jul , 2021

Mbunge wa Jimbo la Ilemela ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula amewataka wananchi kufuata sheria na taratibu za ardhi na mipango miji pindi wanapotaka kujenga ili kujiepusha na hasara zinazoweza kujitokeza ikiwemo kuvunjiwa nyumba zao.

Pichani Mbunge wa Jimbo la Ilemela ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula

Dkt. Mabula amesema hayo akizungumza na wananchi wa kata za Kahama na Kiseke ikiwa ni muendelezo wa ziara yake, ambapo aliwataka wananchi kuhakikisha kabla ya kununua eneo na kulifanyia maendeleo kujiridhisha na matumizi sahihi ya ardhi ya eneo hilo kwa kushirikisha ofisi za ardhi za majiji na Manispaa za eneo husika ili kupunguza migogoro na kuingia hasara.

“Ni marufuku kujenga kiholela katika maeneo yote ya Manispaa kwa sababu yalishatangazwa kama maeneo ya miji, huwezi kufanya uendelezaji wowote bila kuwa na kibali, bila kuwa na ramani, bila kuhusisha ofisi zinazohusika,” amesema Dkt. Mabula.

Sambamba na hilo Dkt. Mabula amewataka wananchi kuacha kununua ardhi kiholela kwani kila kipande cha ardhi kimepangiwa matumizi yake.

Kwa upande wake mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, Afisa Ardhi na Mipango Miji Shukran Kyando amekemea vitendo vya matumizi ya ardhi bila vibali vya Manispaa ikiwemo kuendesha biashara ya ufyatuaji wa matofali katikati ya makazi ya watu jambo linalochangia uharibifu wa mazingira kwa kuzalisha kelele.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa