Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mbowe ajisalimisha polisi

Jumatatu , 20th Feb , 2017

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo na Mbunge wa Jimbo la Hai mkoani Kilimanjaro Mhe. Freeman Aikael Mbowe, leo alasiri amejisalimisha katika Kituo Kikuu cha Polisi Jijini Dar es Salaam.

Freeman Mbowe

Mbowe alitakiwa kuripoti kituoni hapo kwa ajili ya mahojiano kuhusiana na sakata linaloendelea la vita dhidi ya dawa za kulevya.

Taarifa iliyotolewa na chama hicho kupitia mtandao wake wa twitter ilisema "Mh. Freeman Mbowe amekamatwa na polisi waliokuwa wakimfuatilia alipokuwa anaelekea kituo cha polisi kati, mawakili wetu wa chama wako nae".

Taarifa zinadai kuwa Mbowe alishushwa kwenye gari yake akiwa njiani kuelekea polisi, na kupandishwa kwenye gari ya polisi, ambapo baada ya mahojiano kituoni hapo alipelekwa nyumbani kwake kwajili ya kufanyiwa ukaguzi.

Taarifa za kujisalimisha kwa Mhe. Mbowe zimethibitishwa na Msemaji wa Chadema Bw. Tumaini Makene ambaye hakutoa taarifa za undani wa nini kinaendelea hivi sasa ingawa kuna taarifa kwamba baadhi ya viongozi wa juu wa Chadema wanakutana katika kikao cha dharura kujadili suala hilo.

Baadaye majira ya alfajiri, uongozi wa chama hicho kupitia kwa Naibu Katibu Mkuu Salum Mwalimu, ulitoa taarifa za kuachiwa kwa mwenyekiti huyo wa CHADEMA

"Tunapenda kuwatangazia wanachama wetu, wadau,wapenzi na wapenda haki, amani na demokrasia ya kwamba Mwenyekiti Freeman Mbowe ameachiwa huru punde tu mnamo majira ya saa saba na robo usiku huu". Imesema sehemu ya taarifa hiyo.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna wa Polisi Simon Siro ndiye aliyetoa wito wa kumtaka Mhe. Mbowe kuwasili kituoni hapo, ikiwa imepita takribani wiki mbili tangu jina la kiongozi huyo wa Kambi ya Upinzani Bungeni kuwa ndani ya orodha ya watu sitini na tano ambao Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Bw. Paul Makonda amewataka waende kituoni hapo kwa ajili ya mahojiano.

Hata hivyo siku chache baada ya jina lake kutajwa, Mhe Mbowe alikutana na wanahabari nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma na kukana kujihusisha na dawa za kulevya, huku akiweka wazi kuwa kamwe asingekwenda kituoni hapo kwa agizo la Mkuu wa Mkoa bali kwa agizo la Kamanda wa Polisi ambaye kwa maelezo yake ndiye mwenye mamlaka kisheria ya kumwita na kumhoji.

HABARI ZAIDI

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita