Alhamisi , 20th Jul , 2023

Korea Kaskazini haijibu simu za Marekani katika kile kinachoelezwa ni majaribio ya kujadili kuachiliwa kwa mwanajeshi wa Marekani aliyekatiza katika mpaka wake wenye silaha nzito,

Travis King alivuka eneo la mpaka ujulikanao kama DMZ

Washington imesema askari huyo Travis King alivuka eneo la mpaka ujulikanao kama DMZ ,Ukigawanya Korea Kaskazini na Kusini siku ya Jumanne. Msemaji wa wizara ya mambo ya nje Marekani  amesema Pentagon iliwasiliana na Korea Kaskazini lakini simu zao hazipokelewi. 

Korea Kaskazini haijasema lolote juu ya alipo askari huyo na  hatima yake. Mgogoro huo unakuja wakati wa mvutano na Kaskazini. Uhusiano na Marekani umeporomoka katika miaka ya hivi karibuni, kwa kuwa Korea Kaskazini imefanyia majaribio makombora kadhaa yenye nguvu yenye uwezo wa kubeba vichwa vya nyuklia.

Katika ushauri wake wa kusafiri, Marekani inawaambia raia wake wasisafiri kwenda Korea Kaskazini, moja ya majimbo yaliyotengwa zaidi duniani  kutokana na hatari kubwa inayoendelea ya kukamatwa  na tishio muhimu la kuwekwa kizuizini vibaya.