
Travis King alivuka eneo la mpaka ujulikanao kama DMZ
Washington imesema askari huyo Travis King alivuka eneo la mpaka ujulikanao kama DMZ ,Ukigawanya Korea Kaskazini na Kusini siku ya Jumanne. Msemaji wa wizara ya mambo ya nje Marekani amesema Pentagon iliwasiliana na Korea Kaskazini lakini simu zao hazipokelewi.
Korea Kaskazini haijasema lolote juu ya alipo askari huyo na hatima yake. Mgogoro huo unakuja wakati wa mvutano na Kaskazini. Uhusiano na Marekani umeporomoka katika miaka ya hivi karibuni, kwa kuwa Korea Kaskazini imefanyia majaribio makombora kadhaa yenye nguvu yenye uwezo wa kubeba vichwa vya nyuklia.
Katika ushauri wake wa kusafiri, Marekani inawaambia raia wake wasisafiri kwenda Korea Kaskazini, moja ya majimbo yaliyotengwa zaidi duniani kutokana na hatari kubwa inayoendelea ya kukamatwa na tishio muhimu la kuwekwa kizuizini vibaya.