Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mama amuua mwanae kwa moto

Ijumaa , 13th Oct , 2017

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga RPC Benedict Michael Wakulyamba, amethibitisha tukio la mtoto kuungua hadi kufariki kwa moto uliowashwa na mama yake kwaajiuli ya kupikia wilayani Handeni.

RPC Benedict amesema tukio hilo limetokea Oktoba 12 mwaka huu katika kijiji cha Kwamwenda Kata ya Mlorwa Wilaya ya Handeni ambapo mtoto Kessy Kamuje mwenye miaka 3 amefariki kwa kuungua moto akiwa shambani na mama yake mzazi.

“Ni kweli tukio limetokea jana ambapo mtoto Kessy aliungua kwa moto baada ya mama yake kumlaza kwenye kibanda cha nyasi shambani ambacho kilishika moto aliokuwa ameuwasha kwaajili ya kupikia”, amesema RPC Benedict.

Kamanda ameeleza kuwa mama wa mtoto Kessy alifika shambani kwaajili ya shughuli za kilimo ambapo alimlaza mtoto kwenye kibanda cha nyasi na akawasha moto kwaajili ya kupika kisha akaendelea na shughuli za kilimo ndipo Kibanda kikashika moto na kumuunguza hadi kufa mtoto Kessy.

Kwa upande mwingine RPC Benedict amesema madereva kumi wa mabasi waliokamatwa jana kwa kosa la kuendesha kwa mwendokasi kinyume na sheria za usalama barabarani wanarajia kufikishwa mahakamani leo kwaajili ya kujibu mashitaka yanayowakabili.

“Ni kweli tumewakamata madereva 10, baadhi yao wanaendesha mabasi ya abiria yaendayo mikoani, wengine daladala za hapa jijini kwa makosa ya kuendesha mwendokasi na leo watafikishwa mahakamani kujibu mashitaka yao”, amesema RPC Benedict.

HABARI ZAIDI

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe

Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa 124%

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita