
Mama wa watoto waliofariki kwa moto
Akizungumza Mama wa watoto hao amesema haelewi ni kipi kilitokea kwani aliwaacha watoto wake ndani kisha na yeye kwenda sokoni na kwamba hakuwa amewasha kitu chochote na mtungi wa gesi haukuwa na gesi kwani iliisha siku nyingi
Mkaguzi wa Jeshi la Zimamoto Wilaya ya Mpanda George Mwambungu amefika eneo la tukio na amethibitisha kutokea kwa vifo vya watoto hao.
Jeshi la Zimamoto wilayani Mpanda, limetoa rai kwa wazazi na walezi kuacha tabia ya kuondoka nyumbani bila uangalizi wowote kwa watoto wao.