
Jaji Mkuu, Mohamed Chande Othman
Jaji Chande amesema kuwa kati ya hao, 11 ni mahakimu wa mahakama mbalimbali huku wengine 23 ni watendaji wa mahakama na maafisa wa mahakama.
Akizungumza jijini Dar es Salaam mara baada ya kupokea taarifa ya utendaji kazi kwa mahakama hapa nchini Mhe. Chande amesema mahakimu hao pamoja na maafisa wa mahakama wamefukuzwa kazi kutokana na makosa mbalimbali yakiwemo ya utovu wa nidhamu.