Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Jukwaa la wajasiriamali wanawake kuanzishwa Tanga

Ijumaa , 31st Oct , 2014

Wanawake wajasiriamali nchini Tanzania, wametakiwa kujiunga na majukwaa ya wanawake wajasiriamali yaliyopo kwenye mikoa hususani ile ya mipakani, ili wapate fursa ya kubadilishana ujuzi wa kukabiliana na changamoto zinazowakabili katika biashara zao.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Chemba ya Wajasiriamali Wanawake nchini Tanzania (TWCC) Bi. Suzan Mtui.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Chemba ya Wanawake Wajasiriamali nchini Tanzania - TWCC Bi. Suzan Mtui, amesema hayo leo wakati akizungumzia uanzishwaji wa Jukwaa la wajasiriamali wanawake la Horohoro mkoani Tanga, Jukwaa ambalo mara litakapoanzishwa katikati ya wiki ijayo, litakuwa msaada mkubwa kwa ukuaji wa biashara za wajasiriamali wanawake wanaotaka kuuza bidhaa zao katika nchi jirani ya Kenya.

Kwa mujibu wa Bi. Mtui, Jukwaa hilo litawakutanisha akina mama wajasiriamali kutoka mkoa wa Tanga na ile ya jirani, ambapo ametaja moja ya changamoto zitakazotatuliwa kutokana na kuwepo kwa Jukwaa hilo kuwa ni namna ya kufanya biashara nje ya nchi, umuhimu wa vifungashio, upatikanaji wa taarifa muhimu za masoko pamoja na vibali vya mipakani na vile vya kufanya biashara nje ya nchi.

Mkutano wa uundwaji wa jukwaa hilo utafanyika Jumatano wiki ijayo na kwamba baada ya mkutano huo wa Tanga, TWCC itakutana na viongozi wa majukwaa kutoka mikoa yote ya Tanzania kwa lengo la kutoa mafunzo ya uongozi kwa viongozi hao ili wawe msaada kwa wanachama wao hasa umuhimu wa kukuza biashara zao.

Aidha, amesema tangu chemba hiyo ianzishwe miaka miwili iliyopita, biashara zinazomilikiwa na wanawake zimeongezeka na kupata masoko makubwa ndani na nje ya nchi, kwani idadi kubwa ya wanawake wajasiriamali hivi sasa wana ujuzi wa kutafuta masoko pamoja na mbinu za uzalishaji wa bidhaa zenye ubora unaohitajika katika masoko.

Bi. Mtui amesema hata hivyo suala la vifungashio vyenye ubora limekuwa changamoto sio tu kwa wanawake peke yao, bali hata kwa wanaume kwani ukosefu wa vifungashio vyenye ubora limekuwa kikwazo cha upatikanaji wa masoko mazuri ya bidhaa za wajasiriamali hapa nchini.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya