
IGP Simon Sirro
IGP Sirro amesema hayo Dar es Salaam, wakati akizungumza na baadhi ya wananchi wa eneo la Kawe wilayani Kinondoni ambapo amewataka wananchi kuacha kutoa rushwa kwani kitendo hicho ni kinyume na sheria za nchi.
Aidha, IGP Sirro ameendelea kuwasisitiza viongozi wa serikali hasa Watendaji wa Kata na Wenyeviti wa serikali za Mitaa kuwashirikisha wananchi katika vikundi vya ulinzi shirikishi ili maeneo yao yaendelee kuwa salama.