Jumanne , 25th Mei , 2021

Waziri wa TAMISEMI Mhe. Ummy Mwalimu, amesema kuwa katika kuajiri walimu kupitia nafasi za ajira 6,949 zilizotangazwa, serikali itaangalia vigezo zaidi kutoka kwa walimu wanaojitolea, licha ya kwamba wapo ambao wamewasilisha barua feki.

Waziri wa TAMISEMI Mhe. Ummy Mwalimu

Kauli hiyo ameitoa leo Mei 25, 2021, Bungeni Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Longido Dkt. Steven Kiruswa, liliohoji umuhimu wa serikali kuwa ajiri walimu wanaojitolea maeneo yale yale waliyoyazoea.

Aidha Waziri Ummy ameongeza kuwa, Wizara ya TAMISEMI ipo kwenye mtazamo wa kuwafikiria kuwaajiri kwanza wale Walimu waliohitimu tangu mwaka 2012 hadi 2015 na bado hawajaariwa kabla hawajakosa sifa za kuajiriwa na serikali kwani Mwalimu anatakiwa kuajiriwa kabla hajatimiza umri wa miaka 45.

Tazama video hapa chini